#muhitimu: Sehemu ya 1

"Raha jipe mwenyewe"

Nikaifunua tena karatasi yangu ya mtihani katikati, nikaliangalia lile swali ambalo sijalichagua kulijibu na likafanikiwa kuvuta akili na hisia zangu, nikaendelea kulitazama kwa umakini kama nataka kulijibu ila bila wasiwasi wowote kwasababu nimeshamaliza kujibu maswali matano ya uhakika yanayotakiwa na kuyahakikisha kama yako sahihi, wasi wasi wa nini?

Liilikua swali la nne katika ile karatasi ya mtihani, swali la picha au kama liitwavyo “photograph” kuitizama picha ile kwa makini na kisha kujibu maswali yaliyoulizwa, kwa mara ya kwanza picha ya hilo swali iliewekewa rangi katika mtihani wa kidato cha sita. Swali likaendelea kunivuta, japo sikuhitaji kulijibu lakini nilipendezwa sana na picha ya swali hilo.

Ilikua ni picha ya ufukwe mmoja sijui ni wa wapi ila nadhani ni hapa hapa Tanzania, mchanga mwingi, mzuri na laini uliyatenganisha maji na nchi kavu na juu ya ule mchanga kulikua na mstari wa vibanda vya kupumzikia kama 'viduku' ambavyo viliweka kivuli safi, vilikua vya nguzo ya wastani iliyoezekwa kwa majani juu, na chini ya kila kimoja palikua na kiti kama kitanda kidogo kwa ajili ya kujilaza. Mwisho kabisa mwa picha kulikua na watu walioonekana kwa mbali ‘wakila raha’ matumbo nje na hao ndiyo walionivutia.

“Raha jipe mwenyewe” nilikua katika fukwe za malaika siku mbili baada ya mtihani nimejipumzisha juu ya mchanga laini kabisa, miguu inaguswa na mawimbi ya maji yaliyokuwa yanakuja na kuondoka pale ufukweni tulipokaa, sikuwa pekeyangu na pembeni yangu nilikuwa na jirani yangu ambaye tuliongozana mahali pale na tangu tufike alifanikiwa kuyavuta macho ya jamaa iliyofika pale pamoja nasi. Mimi na yule mototo mzuri tulikaa chini ya kivuri kizuri kama vile vijumba vya kwenye mtihani wa jografia tukijiliwaza kwa soda baridi za kopo, biskuti, bajia na vinyama choma tulivyokumbuka kuchukua, tulikua tunatoa uchovu wa mitihani mimi na mama yenu mdogo.

Nikawa naitizama ile miguu yake iliyofunikwa na mtandio uliolowana na sidiria ambayo kama ilikuwa inasukumwa itoke nikawa naona tofauti yangu na wengine ni mimi nilingalia vitu vyangu kwa uhakika wao walikuwa wanachungulia kwa kuibia.

“Ten minitues to time” alinishtua msimamizi akitaja muda uliyobaki tumalize mtihani, na kama nilivyoanza nikahitimisha tena kwa sala nikimshukuru Mungu kwa kuumaliza salama na pia kuomba matokeo mazuri kulingana na jitihada nilizoweka, yaani niliomba nivune nilichopanda. Nikakusanya vitu vyangu, vidogo nikaweka mfukoni, vikubwa nikashika kushoto pamoja na karatasi ya mtihani alafu ya kujibia nikashika kulia nikasimama kwenda kukusanya huku nawaza raha nilizokuwa napata bichi.

............................... itaendelea

Comments

Popular posts from this blog

Become a professional

Graduate V2.0 M-koba account

Become a consultant